Duration 11:48

KAULI YA MAALIM SEIF MBELE YA JPM, MWINYI

206 watched
0
0
Published 14 Jan 2021

KAULI YA MAALIM SEIF MBELE YA JPM, MWINYI MAKAMU wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, .John Magufuli na Rais wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, katika Ikulu Ndogo ya Chato Mkoa wa Geita. Maalim amefika mapema leo Januari, 14, 2021, katika uwanja wa ndege wa Mwanza na kupokelewa na viongozi waandamizi wa serikali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela na Mkoa wa Mwanza, Sevelin Lalika. Pia alipata fursa ya kutembelea ujenzi wa Daraja la Magufuli lililopo Kigongo Feri mpakani mwa Misungwi na Sengerema. Mradi wa daraja hilo ukikamilika utaleta mafanikio makubwa ya kuunganisha baadhi mikoa ya Tanzania na kuunganisha Tanzania na nchi jirani za Burundi, Rwanda na Congo.

Category

Show more

Comments - 0