KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA IBADA YA MORNING GLORY 9/3/2021
UJUMBE WA LEO: "NJIA YAKO DUNIANI"
"YOUR WAY UPON THE EARTH"
NAMNA ROHO ZA WATESI ZINAVYOWEZA KUHARIBU NJIA YAKO DUNIANI
Zaburi 27: 12
Mwanzo 8 : 21
Matendo 12 : 1 - 5
Zaburi 27: 12
12 Usinitie katika nia ya watesi wangu; Maana mashahidi wa uongo wameniondokea, Nao watoao jeuri kama pumzi.
Mathayo 14 : 1 - 12
1 Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake,
2 Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake.
3 Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.
4 Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.
5 Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii.
6 Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode.
7 Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba.
8 Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.
9 Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe;
10 akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani.
11 Kichwa chake kikaletwa katika kombe, akapewa yule kijana; akakichukua kwa mamaye.
12 Wanafunzi wake wakaenda, wakamchukua yule maiti, wakamzika; kisha wakaenda wakampasha Yesu habari.
Mwanzo 8 : 21
21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya.
Matendo 12 : 1 - 5
1 Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.
2 Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.
3 Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa.
4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.
5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
Mhubiri 10 : 5 - 9
5 Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye;
6 ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa.
8 Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.
9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo; Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.
Yeremia 1 : 4 - 5
4 Neno la Bwana lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Maombolezo 3 : 9 - 17
9 Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.
10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni.
11 Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa.
12 Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
13 Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake.
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa.
15 Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga.
16 Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu.
17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.
Mhubiri : Mwl. Emilian Katubayemo
Kwa maombi na ushauri:
Mch. Dkt. Eliona Kimaro.
Simu :+255655516053, +255754516053
YouTube : Rev. Dr. Eliona Kimaro TV
Barua Pepe: elionakimaro555@gmail.com
Category
Show more
Comments - 41
Related videos for KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA IBADA YA MORNING GLORY :