Duration 55:6

KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA IBADA YA MORNING GLORY

7 043 watched
0
135
Published 9 Mar 2021

KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA IBADA YA MORNING GLORY 9/3/2021 UJUMBE WA LEO: "NJIA YAKO DUNIANI" "YOUR WAY UPON THE EARTH" NAMNA ROHO ZA WATESI ZINAVYOWEZA KUHARIBU NJIA YAKO DUNIANI Zaburi 27: 12 Mwanzo 8 : 21 Matendo 12 : 1 - 5 Zaburi 27: 12 12 Usinitie katika nia ya watesi wangu; Maana mashahidi wa uongo wameniondokea, Nao watoao jeuri kama pumzi. Mathayo 14 : 1 - 12 1 Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake, 2 Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake. 3 Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye. 4 Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye. 5 Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii. 6 Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode. 7 Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba. 8 Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji. 9 Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe; 10 akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani. 11 Kichwa chake kikaletwa katika kombe, akapewa yule kijana; akakichukua kwa mamaye. 12 Wanafunzi wake wakaenda, wakamchukua yule maiti, wakamzika; kisha wakaenda wakampasha Yesu habari. Mwanzo 8 : 21 21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya. Matendo 12 : 1 - 5 1 Panapo majira yale yale Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. 2 Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga. 3 Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro. Siku hizo zilikuwa siku za mikate isiyochachwa. 4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. 5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Mhubiri 10 : 5 - 9 5 Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye; 6 ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini. 7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa. 8 Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma. 9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo; Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo. Yeremia 1 : 4 - 5 4 Neno la Bwana lilinijia, kusema, 5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Maombolezo 3 : 9 - 17 9 Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu. 10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni. 11 Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa. 12 Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale. 13 Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake. 14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa. 15 Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga. 16 Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu. 17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa. Mhubiri : Mwl. Emilian Katubayemo Kwa maombi na ushauri: Mch. Dkt. Eliona Kimaro. Simu :+255655516053, +255754516053 YouTube : Rev. Dr. Eliona Kimaro TV Barua Pepe: elionakimaro555@gmail.com

Category

Show more

Comments - 41